Falsafa za Enock Maregesi: Nukuu za Nyakati Zetu

· DL2A - BULUU PUBLISHING
5.0
3 reviews
Ebook
446
Pages
Eligible
Ratings and reviews aren’t verified  Learn More

About this ebook

Kitabu cha Falsafa za Enock Maregesi: Nukuu za Nyakati Zetu ni mkusanyiko wa nukuu za Enock Maregesi, kila nukuu kuu na maana yake, kila siku na nukuu yake kwa mwaka mzima. Ni mkusanyiko wa nukuu kuu 365 zenye kuleta hamasa na msukumo wa mafanikio katika maisha ya mtu.

Lengo la kitabu hiki ni mtu kuwa na nukuu katika kila jambo katika kila hali katika kila kipengele cha maisha yake, kupata amani ya moyo na uhuru wa nafsi, kama msingi wa mafanikio, katika maendeleo ya maisha yake kwa ujumla wake.

Ukitaka kujitambua katika maisha yako jijibu maswali yafuatayo: Wewe ni nani? Umetoka wapi? Kusudi la maisha yako ni nini hapa duniani? Kisha tengeneza dira ya maisha ya nyuzi 360 inayozidi hata hatima ya maisha yako ya hapa.

Kitabu cha Falsafa za Enock Maregesi: Nukuu za Nyakati Zetu kitakusaidia kutengeneza dira ya maisha inayozidi maisha yako ya hapa duniani. Aidha, kitakusaidia kupata angalau nukuu 12 za kwako mwenyewe zitakazokuongoza na kukupeleka katika mafanikio yako ya kimwili na ya kiroho pia.


Ratings and reviews

5.0
3 reviews
Enock Maregesi
January 22, 2021
Falsafa za Enock Maregesi: Nukuu za Nyakati Zetu is a collection of selected quotes from the writings of Enock Maregesi, award-winning author of Kolonia Santita, in Kiwahili language and edited by Dr Mathieu Roy of DL2A Buluu Publishing & Software Development based in Paris, France. This book is made up of 365 commented quotes which aim to give motivation and inspiration towards success and personal fulfillment. The purpose of this book is to provide at least a quote for every aspect of a person's life so that they may achieve peace of soul and spiritual liberation. That is, to provide the basis for success in one's life as a whole. In order to know yourself, you have to answer the following questions: Who are you? Where are you from? What is the purpose of your life in this world? Then create a 360° vision of your life, a vision that goes beyond the end of your life in this world.
1 person found this review helpful
Did you find this helpful?

About the author

Mwandishi Enock Abiud Maregesi alizaliwa nchini Tanzania katika mkoa wa Mwanza mnamo mwaka 1972, Novemba 25. Alisomea teknolojia ya habari na utawala wa biashara katika Chuo Kikuu cha Wales, na uandishi wa habari na vitabu katika chuo cha fasihi ya ubunifu cha The Writers Bureau, nchini Uingereza. Alisomea pia sayansi ya roho ya Kabala katika Taasisi ya Bnei Baruch ya Petah Tikva nchini Israeli.

Mnamo mwaka 2015 kitabu chake cha kwanza, Kolonia Santita: Laana ya Panthera Tigrisi, kilishinda Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Afrika; iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Cornell cha New York, Marekani, na kampuni ya Mabati Rolling Mills ya Nairobi nchini Kenya. Anaishi jijini Dar es Salaam, Tanzania, anakojishughulisha na biashara na uandishi wa vitabu.


Kitabu kilihaririwa na Dkt Mathieu Roy aliyepata shahada ya kwanza ya falsafa ya chuo kikuu cha La Sorbonne, Paris, Ufaransa pamoja na shahada ya kwanza ya teknolojia ya habari baada ya masomo ya hisabati, biolojia, falsafa na teknolojia ya habari. 

Alikutana na lugha ya Kiswahili, nchini Tanzania mwanzoni mwa mwaka 2000. Huba ya kujua Kiswahili ikampanda hasa upande wa mashairi na fasihi kwa jumla. Akapata shahada ya uzamili ya Kiswahili na shahada ya uzamivu ya Kiswahili kwenye Chuo Kikuu cha INALCO – Paris Sorbonne Cité. Tasnifu yake ya uzamivu inahusu kanuni za kutunga mashairi na ushairi wa Mathias E. Mnyampala. Anajishughulisha na uhariri wa vitabu vinavyoandikwa kwenye lugha ya Kiswahili, utafiti na teknolojia ya habari. Anaishi kati jiji la Paris na Dar es-Salaam, Tanzania.


Rate this ebook

Tell us what you think.

Reading information

Smartphones and tablets
Install the Google Play Books app for Android and iPad/iPhone. It syncs automatically with your account and allows you to read online or offline wherever you are.
Laptops and computers
You can listen to audiobooks purchased on Google Play using your computer's web browser.
eReaders and other devices
To read on e-ink devices like Kobo eReaders, you'll need to download a file and transfer it to your device. Follow the detailed Help Center instructions to transfer the files to supported eReaders.